Wakala
 ya Mkemia Mkuu wa Serikali imekusudia kuendesha kampeni maalum ya 
kupima matumizi ya vilevi kwa madereva wanaosafirisha abiria na mizigo 
ikiwa ni hatua ya kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani nchini.
Hayo
 yamesemwa jana Jijini Dar es Salaam na Mkemia Mkuu wa Serikali Profesa 
 Samwel Manyele alipokuwa akifungua mafunzo ya siku mbili kwa wadau wa 
kemikali juu ya matumizi salama ya kemikali nchini.
Profesa
 Manyele alisema utaratibu wa kuwapima madereva hao utaanza hivi 
karibuni na utawezesha kupunguza tatizo la ajali barabarani na kuvitaka 
vyombo vya ulinzi na usalama kutoa ushirikiano katika zoezi hilo.
“Madereva
 wote wanaosafirisha mizigo na abiria watatakiwa kupita kwenye kipimo 
ambacho kitaonyesha kama madereva hao wanatumia vilevi, hali hiyo 
itasaidia kutatua tatizo la ajali za barabarani nchini”, alisema Manyele.
Profesa 
 Manyele alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kutoa uwezo na uelewa kwa
 wahusika  hasa wasimamizi wa shughuli za kemikali na matumizi salama 
juu ya kukabiliana na matukio au ajali za kemikali pale yanapotokea.
Sign up here with your email

ConversionConversion EmoticonEmoticon