Wananchi wampa Majaliwa siri nzito



 
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amesema wananchi kutumia mabango kueleza kero zao ni ushahidi kwamba watendaji na madiwani hawawapi nafasi ya kueleza shida zao.
Majaliwa amesema kwa kutambua hawana nafasi ya kuuliza maswali, wananchi walitumia mabango katika kila mkutano aliohutubia ili kutoa waliyonayo moyoni.
Akizungumza katika mkutano wa kuhitimisha ziara yake mkoani Arusha, Waziri Mkuu alisema ni wazi kuwa viongozi wa serikali ngazi ya wilaya, kata na vijiji hawaandai mikutano na kuzungumza nao.
“Endapo mngekuwa mnaandaa mikutano ya hadhara, wananchi wasingeomba kujua lini watapata kiwanja cha kujenga kanisa lao mbele ya Waziri Mkuu,” alisema.
Kwa habari zaidi nunua nakala yako ya NIPASHE LEO
Previous
Next Post »

COMMUNITY HELP