Mwanamke aliyepata mtoto London kwa kutumia tishu za ovari zilizogandiswa akiwa mtoto ameelezea kuzaliwa kwa mtoto wake kama muujiza.
Inasemekana kuwa hii ni mara ya kwanza kwa madaktari popote ulimwenguni kutumia utaalam kama huo kuweza kupata mtoto.
Madaktari wake wanasema kuwa mafanikio hayo yatatoa matumaini zaidi kwa watoto wengine wenye tishu za ovari zilizohifadhiwa kabla ya kufanyiwa matibabu ya saratani.
Mtoto wa Moaza alizaliwa katika hospitali ya London
Moaza Al Matrooshi,mwenye asili ya Dubai, alizaliwa na matatizo ya mfumo kwenye damu yaliyomfanya asiweze kuzaa akiwa mtu mzima ambapo tishu za ovari zake zilichukuliwa na kuhifadhiwa na wataalam hao wa afya ili kuchanganya na mayai yake atakapokuwa mkubwa kisha kupatikana kwa mtoto.
Tishu za ovari za Moaza zilivyochukuliwa na kuhifadhiwa
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon