Waziri
 Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amevunja ukimya kuhusu mgogoro wa 
uhalali wa Uenyekiti wa Profesa Ibrahim Lipumba anayetambuliwa na Ofisi 
ya Msajili wa Vyama vya Siasa unaoendelea ndani ya Chama Cha Wananchi 
(CUF) ambao umekuwa ukihusishwa naye tangu awali.
Lowassa
 ambaye alitajwa na Profesa Lipumba kuwa chanzo cha yeye kujiuzulu kabla
 ya kurejea tena miezi 9 baadae kutengua uamuzi wake, amesema kuwa shida
 za chama hicho ni shida za vyama vyote vinavyounda Ukawa.
Mwanasiasa
 huyo mkongwe na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, ametumia ukurasa wake 
wa Facebook kueleza jinsi ambavyo Ukawa inalibeba tatizo la mgogoro wa 
CUF.
“CUF
 ni wenzetu katika Ukawa. Shida zao ni shida zetu, vita vyao ni vita 
vyetu, kushindwa kwao ni kushindwa kwetu, ushindi wao ni ushindi wetu,” aliandika Lowassa.
Kauli
 hiyo ya Lowassa imekuja miezi michache baada viongozi wa Ukawa kueleza 
msimamo wao kuwa hawamtambui Profesa Ibrahim Lipumba kama Mwenyekiti wa 
CUF na kwamba wataendelea kushirikiana na Katibu Mkuu wa Chama hicho, 
Maalim Seif Sharif Hamad.
Naye Profesa Lipumba amekuwa akieleza kuwa hayuko tayari kuona Chadema au Lowassa wanakinunua chama hicho.
Hivi karibuni, Ukawa wameweka msimamo wao kuwa watawasimamisha wagombea wa pamoja katika uchaguzi mdogo utakaofanyika mwakani.
Hata
 hivyo, kumekuwa na changamoto baada ya pande mbili zinazovutana ndani 
ya CUF kila mmoja kutangaza kuwasimamisha wagombea wake huku Tume ya 
Taifa ya Uchaguzi ikiweka msimamo kuwa ili iwatambue wagombea wa chama 
hicho ni lazima fomu zao zisainiwe na pande mbili zinazovutana.
Miezi
 michache kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, Profesa 
Lipumba alionekana akimtambulisha Lowassa mbele ya waandishi wabari na 
kujibu maswali mengi yaliyoelekezwa kwake lakini siku chache baadae 
alitangaza kujiuzulu akida moyo wake unamsuta hawezi kumuunga mkono 
mwanasiasa huyo.
Sign up here with your email

ConversionConversion EmoticonEmoticon