Miaka 40 toka kuanzishwa kwa kijiji hawakuwahi kuona barabara

Wananchi wa kijiji cha Kingole wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma wamesema kwa Zaidi ya miaka arobaini toka kuanzishwa kwa kijiji hicho hawakuwahi kupata barabara hali iliyowalazimu wagonjwa wakiwemo akina mama wajawazito kutembea kwa miguu takriban kilomita 30 kufuata huduma za matibabu.
screen-shot-2016-11-14-at-10-34-31-am
Kero ya ukosefu wa barabara imeghalimu maisha ya wananchi wengi ambao wamepoteza maisha kwa kufia njiani kwa sababu ya kuchelewa kupata matibabu.
Wananchi hao wamesema baada ya kufikisha kilio chao kwa viongozi wenye dhamana ya kulinda maisha yao miaka mitatu iliyopita wakala wa barabara TANRODS mkoa wa Ruvuma wamejenga barabara kutoka Peramiho hadi Kingole kwa kiwango cha changalawe kupitia channel ten wameishukuru serikali ya mkoa wa Ruvuma kwa kusikia kilio chao.
Mhandisi wa TANRODS mkoa wa Ruvuma Lazeck Alinanuswe amekili kuwa barabara ya Kingole haikuwahi kujengwa lakini sasa wananchi hao watasahau shida zao baada ya serikali kutoa fedha za ujenzi wa barabara ya kilomita 80.
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dkt.Binirithi Saatano Mahenge ametembelea barabra hiyo kutoka Peramiho hadi Kingole ili kujiridhisha kama imejengwa kwa kiwango kinachotakiwa kabla ya mvua haijanyesha.
Mkoa wa Ruvuma una wilaya sita Halmashauri saba na vijiji Zaidi ya 540 Geofrey Nilahi Channel ten Songea.
Previous
Next Post »

COMMUNITY HELP