Mamlaka 
 ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) imetangaza kuanzishwa kwa 
mfumo mpya wa ukataji wa tiketi za mabasi na daladala kwa njia ya 
kielektroniki.
Hatua
 hiyo ina lengo la kurahisisha upatikanaji wa mapato halali ya serikali 
pamoja na kuwafanya madereva na makondakta, kuajiriwa rasmi na wamiliki 
wa vyombo hivyo vya usafiri.
Pia
 mamlaka hiyo imezindua kampeni ya usafi kwa wafanyakazi wa daladala, 
ambayo inawataka kubadilisha sare za madereva na makondata, ambazo 
walishonewa na matajiri wao.
Sasa wafanyakazi hao watashona sare zao wao wenyewe ili wawe na uhalali wa kuzimiliki na kuzifanyia usafiri wa mara kwa mara.
Mkurugenzi
 wa Barabara wa Sumatra, Johansen Kahatano alisema jana kuwa mfumo huo 
wa tiketi za daladala kwa njia ya elektroniki, utaanza kutumika Januari 
mwakani.
Lakini, aliongeza kuwa kuanzia Desemba mwaka huu, watafanya mpango huo kwa majaribio kwa mabasi yaendayo mikoani.
“Kwa
 sasa tumeanza mpango huo kwa majaribio kwa daladala za kampuni ya 
Christian, Desemba tutaenda kwa mabasi ya mikoani na Januari mwaka 
kesho, mfumo huo utaanza kwa mabasi na daladala zote,” alisema Kahatano.
Alitangaza
 mfumo huo jana wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usafi kwa madereva, 
ambayo inahusisha usafi wa mwili, mavazi na mabasi uliofanyika katika 
stendi ya Makumbusho, Dar es Salaam. Katika kampeni hiyo, madereva na 
makondakta watajishonea wenyewe sare zao na sio wamiliki wa magari.
Kahatano
 alisema chini ya mfumo wa ukataji wa tiketi kwa njia ya kielektroniki, 
utamfanya mmiliki wa basi kujua mapato yake halisi kwa siku na hivyo 
atawalipa wafanyakazi wake mshahara na Serikali itapata kiwango sahihi 
cha kodi. Kwa sasa ukataji wa tiketi za mabasi na ule wa daladala, 
unafanywa kwa tiketi zilizochapishwa.
Alisema kutokana na mfumo huo mpya, dereva haruhusiwi kumlipa mmiliki hesabu ya kila siku kama wanavyofanya sasa.
Badala
 yake, mmiliki ndiye atatakiwa kumlipa dereva na kondakta wa gari lake 
mshahara kila mwisho wa mwezi. Alisema ili malipo hayo yaweze kufanyika 
ni lazima madereva waajiriwe rasmi na walipwe chini ya mfumo wa ajira.
“Kwa
 hiyo dereva na mmiliki wataingia mkataba wa ajira tofauti na sasa hivi 
hakuna mkataba wowote kati ya tajiri na wafanyakazi wake, badala yake 
wanakubaliana tu kwamba hesabu ya siku ni kiasi fulani cha fedha na 
dereva anahangaika kukitafuta,” alisema Kahatano.
Kuhusu
 sare za madereva, alisema kwamba ndani ya wiki mbili madereva wa wilaya
 ya Kinondoni, wote wanatakiwa wawe wamebadili sare zao na kushona 
ambazo wamekubaliana na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi 
(VETA).
Mkuu
 wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Awadhi
 Haji, alisema wao kama wasimamizi wa sheria, watahakikisha ndani ya 
wiki mbili madereva wote wa daladala wa wilaya ya Kinondoni, wanashona 
sare hizo mpya ambazo zimepitishwa na Sumatra.
Alisema
 kutokana na agizo hilo, hategemei kuwaona tena makondakta na madereva 
wachafu kwa kuwa watakuwa na sare zao binafsi ambazo watazitunza kuliko 
ilivyokuwa awali.
“Wale ambao watakaidi tutawakamata na kuwafikisha mahakamani.”
Sign up here with your email

ConversionConversion EmoticonEmoticon