Panda Mbegu Ya Mafanikio Yako Leo

Inawezekana upo kwenye wakati mgumu sana kimaisha ukiwa huna pesa, mipango yako inakwenda hovyo na huna uhakika hata hiyo kesho yako itakuwa vipi yaani ni kipi utakula na kipi utavaa.

Kila njia unayowaza kwamba inaweza kukuingizia kipato bado unaona pia nayo kama vile haikusaidii sana. Ukiangalia kila mlango unaoufahamu wewe wa kukupa pesa kama haupo na hata wale wateja wako umewapoteza.

Hali kama hizi ni hali ambazo zinamkuta karibu kila mtu duniani. Kuna mahali katika maisha yako ni lazima itafika utajikuta upo njia panda kwa sababu ya mambo yako kwenda hovyo hovyo.

Inapotokea hali kama hiyo mifuko imechacha yaani huna mapesa, kitu kikubwa cha kufanya badala ya kusikitika, anza kupanda upya mbegu ya mafanikio yako tena. Ni wakati wa kuhakikisha unapanda mafanikio yako ili kesho uvune.

Kwa jinsi utakavyozidi kupanda mbegu nyingi za mafanikio leo ndivyo utajikuta unavuna sana kesho. Kama unalalamikia leo maisha yako ni magumu, hebu jiulize ulipanda nini unachotaka kuvuna leo.

Tukiangalia hakuna ulichokipanda. Kama hukupanda kitu, kaa kimya anza kuweka mikakati na mipango yako upya ya kimaisha itakayokupa mafanikio makubwa kesho. Kila kitu kinawezekana ukiamua.
Previous
Next Post »

COMMUNITY HELP