Serikali  inakamilisha Muswada wa Sheria utakaoweka wazi sifa za walimu wakiwamo wa vyuo vikuu, msingi na sekondari nchini.
Hayo
 yalisemwa jana na Waziri wa Elimu, Sayansi , Teknolojia na Mafunzo ya 
Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako katika kongamano la kujadili hali 
halisi ya elimu nchini lililoandaliwa na walimu wastaafu.
Profesa
 Ndalichako alisema   serikali pia inaandaa  mpango wa kuanzisha chombo 
maalum cha kitaaluma kitakachosimamia walimu kwa mujibu wa sheria.
Alisema muswada huo utakapokuwa tayari utawasilishwa bungeni.
Alisema 
 pamoja na mambo mengine, utataja sifa za mwalimu mkuu na mkuu wa chuo  
kuondoa dhana kwamba ualimu ni kazi ya walimu mazoea.
“Ni lazima kuwe na sheria inayoweka wazi sifa ya mwalimu mkuu wa chuo kikuu na sifa za kuweza kujiunga na chuo cha ualimu.
“Siyo kuweka tu sheria zisizojieleza hali ambayo imesababisha taifa kuwa na wasomi wasiokuwa na sifa.
“Ili
 tuweze kufikia katika mpango wa kutoa elimu bora ni lazima tuchukue 
hatua zinazostahiki kwa manufaa ya taifa ingawa unapochukua hatua 
Watanzania wengi wanalalamikia suala hili ila ukweli utabaki kuwa 
ukweli.
“Nchi haiwezi kuendeshwa na walimu wasiokuwa na sifa kwa sababu kitakachozalishwa pia kitakuwa ni mtihani na aibu kwa nchi.
“Kama
 kuna mwalimu yeyote ambaye anajijua hana sifa na amekalia kiti hicho 
kwa zaidi ya miaka 10 atambue kuwa hicho kiti atakiacha.
“Serikali hii ya awamu ya tano hatutaki kuwa na walimu wasiokuwa na sifa, bora kujiengua mwenyewe,”alisema Profesa Ndalichako.
Waziri  
 alisema changamoto kubwa inayoikabili wizara yake ni utekelezaji wa 
mipango endelevu ya wizara ambayo ni mizuri lakini utekelezaji wake ni 
mdogo kutokana na kuingiliana kwa mipango ya maendeleo endelevu.
Sign up here with your email

ConversionConversion EmoticonEmoticon