Muonekano wa Hospitali ya Kisasa iliyoko Mloganzila DSM yenye ghorofa tisa By Edwin Kamugisha TZA on October 12, 2016





 ctober 11 2016 Mabalozi wa Jamhuri ya Muuungano ya Tanzania walioko nchi za nje walitembelea hospitali ya Kisasa kujionea Ujenzi wa kampasi ya chuo na hospitali ya taaluma na tiba ya chuo kikuu cha afya na sayanzi shirikishi, Muhimbili. 
Hospitali hiyo ipo Mloganzila Dar es salaam, kitu cha kufahamu ni kuwa itakuwa na ghorofa tisa, vyumba vya upasuaji kumi, mashine za kufanyia uchunguzi za kisasa, wodi za kulaza wagonjwa karibu flow tano za kisasa na wodi zingine. Makamu mkuu wa chuo Prof. Ephata Kaaya kaelezea mambo muhimu ambayo kampasi ya chuo na hospitali ya Taaluma na Tiba, ya chuo kikuu cha afya na sayanzi shirikishi, Muhimbili itakuwa nayo………..
>>> ‘Kampasi hii ikikamilika, chuo kitaweza kuongeza udahili wa wanafuzni kutoka 4,000 waliopo sasa hadi 15,000, kufanya tafiti nyingi zenye ubora na zinazolenga matatizo ya wananchi wetu na kutoa huduma za afya kwa kiwango cha juu kwa wananchi’
>>>’Hospitali hii ni ya kisasa na itatoa huduma za afya za hali ya juu, mafunzo bora kwa wanafunzi wa fani ya afya, uchunguzi wa magonjwa na tafiti zenye ubora katika fani za afya hapa nchini. Itakapoanza kutumika, hospitali hii itapunguza kwa kiasi idadi ya wagonjwa na gharama zinazotumika kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu’;- Prof. Ephata Kaaya
Previous
Next Post »

COMMUNITY HELP